Friday, September 23, 2016

NAVY KENZO WAJAWA FURAHA BAADA YA KUTAJWA KUWANIA MTV MAMA AWARDS 2016.

 Majina ya wasanii watakaowania tuzo za MTV MAMA 2016 yalitajwa huku Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz na kundi la Navy Kenzo  ndio wasanii wa Tanzania waliotajwa kuwania tuzo kubwa za Africa za MTV Africa Music Awards 2016. Navy kenzo  waeleza  furaha  yao  baada  ya  kutajwa  kuwania  kipengele  cha  kundi  bora  la  mwaka  kwenye  tuzo  hizo.
"Tunashukuru sana tumepata taarifa za MTV MAMA 2016 tumechaguliwa kwenye Best Group yaani tumefurahia sana ni kitu ambacho kimetutia nguvu sana
Kimeonesha jinsi gani kazi yetu ambayo tuliyokuwa tukifanya kwa muda mrefu ndio imeanza kuleta matunda hayo kwahiyo tunashukuru sana, tutatoa maelekezo katika mitandao yetu ili mashabiki wetu na wengineo wajue jinsi ya kutupigia kura"

No comments:

Post a Comment